Tuesday 2 January 2018

Matumizi ya bangi yahalalishwa California

California limekuwa jimbo kubwa zaidi nchini Marekani kuhalalisha matumizi ya bangi kwa burudani.

Kuanzia sasa Januari mosi mwaka 2018 watu walio na umri wa kuanzia miaka 21, wanaweza kumiliki hadi gramu 28 za bangi na kupanda hadi miti 6 ya bangi nyumbani.
Wanaopinga wanasema kuwa sheria hiyo itasababisha watu kuendesha magari wakiwa tayari wamevuta bangi kuchangia vijana kuvuta bangi.
Lakini biashara zinatabiri kile kinaonekana kuwa sekta ya mabilioni ya dola miaka michache inayokuja.
Wakaazi wa Califonria walipigaa kura kuunga mkono kipengee cha kuhalalisha bangi miaka 14 iliyopita katika kura ambayo ilifanyika sambamba na uchaguzi wa rais nchini humo.
Tangu wakati huo sheria ngumu zinazohusu kodi zimeandikwa kudhibiti mauzo ya bangi.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni ambayo inafuatilia soko la bangi duniani alitabiri kuwa kutakuwa na kushuka kwa bei kwa mwaka wa kwanza au miaka miwili.
Hata hivyo, faida ni kubwa katika jimbo hilo tajiri zaidi na lenye watu wengi zaidi nchini Marekani.
Mwaka 1996, California lilikuw jimbo la kwanza kuhalalisha bangi kwa matumizi ya matibabu.
Inakadiriwa kuwa soko la bangi haramu kwa sasa ni dola milioni 5.1 na wakati itahalalishwa thamani yake itakuwa ya dola bilioni 5.8 itakapofikia mwaka 2021.

0 comments:

Post a Comment