Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’
amesema licha ya kuwa bado ana hofu, kesho anarejea Uganda kutoka
Marekani alikoenda kupatiwa matibabu, amesema wasiwasi alionao hata
Waganda milioni 44 pia wanao na Uganda ndiko iliko familia yake na watu
wake hivyo lazima arudi.
Kimetua
nchini humo leo na kupiga eneo la Guangdong ambalo ni eneo lenye watu
wengi zaidi huku kikitishia kuleta madhara makubwa Hong Kong na Macau - Kinasafiri
maili 170 kwa saa na kwa mujibu wa shirika la kutoa tahadhari za
vimbunga la Marekani mwendokasi huo ni mara mbili ya Kimbunga Florence
kinachotishia pwani ya Marekani - Aidha, kwenye pwani ya China
vinu viwili ya Nyuklia, Yangjiang na Taishan vimeonekana kuwepo katika
njia ya Kimbunga hicho lakini Mamlaka katika kinu cha Yangjiang imesema
ipo tayari na imejizatiti kujilinda - Kwa upande mwingine, daraja
refu zaidi duniani linalokatisha baharini lenye urefu wa maili 34
lililogharimu dola za Kimarekani Bilioni 20 lipo hatarini kutokana na
kukatiza kwenye Bahari ya Kusini ya China ambapo Kimbunga hicho kinapita - Daraja
hilo linalounganisha Hong Kong, Macau na Zhuhai lilitengenezwa kukaa
miaka 120, kuhimili upepo wa kasi ya maili 120 kwa saa na tetemeko la
ardhi lenye ukubwa wa Kipimo cha tetemeko richa 8
Kupitia
msemaji wake Ofono Opondo yautaka Muunganiko huo wa Ulaya kutatua
matatizo yake kwanza na kuacha kuingilia masuala ya bara la Afrika - Yasema haitakubali Umoja wa Ulaya kuishurutisha kufanya masuala yasiyouhusu na kuwa Uganda ina mifumo yake ya kujitawala - Aidha,
imesema kuwa uhasama wake na EU ni kutokana na kushindwa kuidhinisha
ndoa za jinsia moja na uhusiano wake na nchi ya China - Kauli hizo
zinakuja ikiwa ni baada ya EU kuitaka Serikali ya Museveni kuheshimu
haki, demokrasia na Mihimili mingine ya Serikali ikiwemo Bunge
Rais Paul Kagame ametumia uwezo wake Kikatiba kuwaachia huru wafungwa 2,000 waliokuwa wamefungwa kwa makosa kadhaa ya uhalifu - Miongoni
mwa wafungwa hao ni Mwanamuziki, Kizito Mihigo aliyekuwa akihudumia
kifungo cha miaka 10 na Kiongozi wa Upinzani, Victoire Ingabire
aliyekuwa akihudumia kifungo cha miaka 15 tangu 2010 - Bi.
Ingabire alirudi kutoka jela nchini Uholanzi mwaka 2010 ili kushiriki
katika uchaguzi wa urais lakini alikamatwa na kuzuiliwa kuwania urais - Aidha,
ni Hutu aliyekuwa akihoji ni kwanini makumbusho ya mauaji ya halaiki
nchini humo ya mwaka 1994 hayakuhusisha watu wa kabila la Hut
Jeshi
la Polisi linamshikilia Askofu Franco Mulakkal wa Kanisa Katoliki
Dayosisi ya Kaskazini mwa Jimbo la Punjab nchini India anayetuhumiwa kwa
ubakaji. - Anatuhumiwa kufanya matukio hayo katika kipindi cha mwaka 2014 hadi 2016 - Watawa
walifanya mgomo kwa siku kadhaa wakishinikiza kukamatwa kwake. Mgomo
huo ulijumuisha makundi ya Wanaharakati na Watetezi wa haki za Wanawake
Maafisa
Usalama wa Uganda wazuia jaribio la mamlaka za Kenya la kutaka
kupandisha bendera ya nchi yao katika Kisiwa hicho kinachobishaniwa - Waganda
wameshusha bendera hiyo iliyopandishwa na Wakenya na kutoa onyo la
kuwataka wasirudie kitendo hicho walichokiita ni chokochoko - Serikali
ya Kenya na Uganda zimekuwa kwenye mgogoro kuhusu umiliki wa kisiwa
hicho kilichopo ndani ya Ziwa Victoria tangu mwaka 2004
University College London ni cha 18. Kwa kuangazia sifa za vyuo vikuu
miongoni mwa waajiri, Cambridge na Oxford ndivyo vinavyoongoza, lakini
kwa jumla vyuo vikuu vya Uingereza vilishuka katika ushirikiano na
waajiri na viwango vya kuajiriwa kwa wanafunzi wao.
Kuimarika kwa China kunadhihirishwa na kuorodheshwa kwa Tsinghua University nafasi ya tisa na University of Peking nafasi ya 20.
Kati
ya vyuo vikuu 500 vilivyoorodheshwa, 102 vinatoka bara Asia, 144 kutoka
Ulaya Magharibi. Marekani ina vyuo vikuu 83, ambapo 13 kati ya vyuo
hivyo vimo katika orodha ya 30 bora. Afrika kuna vyuo vikuu 10.
Chuo
hicho kikuu cha Nairobi ndicho pekee kutoka Afrika Mashariki ingawa
kimeshuka kutoka nambari tano Afrika mwaka 2018, mwaka ambao kulikuwa na
vyuo vikuu 11 vya Afrika katika vyuo vikuu 500 bora duniani kwenye
orodha hiyo. Vyuo Vikuu vinavyopendwa na waajiri Afrika 2019
University of Cape Town, Afrika Kusini
The American University in Cairo, Misri
University of Witwatersrand, Afrika Kusini
Cairo University, Misri
Ain Shams University, Misri
Stellenbosch University, Afrika Kusini
University of Johannesburg, Afrika Kusini
University of Kwazulu-Natal, Afrika Kusini
University of Nairobi, Kenya
University of Pretoria, Afrika Kusini
Chuo kikuu cha Alexandria cha Misri ndicho kilichotupwa nje
katika orodha ya mwaka huu baada ya kuwa nambari nane Afrika mwaka
uliopita.
Chuo
kikuu cha Cape Town ambacho kinaongoza Afrika katika orodha ya jumla
kinashikilia nafasi ya 101-110, na hakuna chuo kingine cha Afrika hadi
baada ya vyuo mia ambapo ndipo unapata chuo kikuu cha Kimarekani cha
Cairo na Chuo Kikuu cha Witwatersrand cha Afrika Kusini katika nafasi ya
201-250.
Chuo Kikuu cha Nairobi kinashikilia nafasi ya 301-500. Mwaka jana, kilikuwa katika nafasi ya 251-300 kwa jumla.
Mwaka
2017, Afrika ilikuwa na vyuo vikuu vinne pekee, wakati huo orodha hiyo
kwa jumla ikishirikisha vyuo vikuu 300 duniani. Mwaka 2017
walishirikisha vyuo 494 na mwaka huu vyuo 497.
Vyuo vikuu 30 bora duniani kwa kupendwa na waajiri
Hatua
hii ni matunda ya makubaliano ya amani yaliyosainiwa na Waziri Mkuu wa
Ethiopia, Abiy Ahmed na Rais wa Eritrea, Isaias Afwerki mwezi Julai 2018 - Ethiopia imeahidi kuanza kuviondoa vikosi vyake katika mpaka wake na Eritrea - Mataifa
hayo yaliingia kwenye mgogoro uliosababisha vita kati yao kuanzia mwaka
1998-2000. Vita hiyo ilisababisha baadhi ya familia kutengana
Rais
wa Ghana, Nana Akufo-Addo aongoza mamia ya waombolezaji kuupokea mwili
wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN), Kofi Annan uliowasili
nchini humo ukitokea Jijini Geneva nchini Uswisi - Annan aliyewahi kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel(2001), alifariki Agosti 18 mwaka huu baada ya kuugua kwa muda mfupi - Annan aliongoza Umoja wa Mataifa kuanzia Januari 1997 hadi Desemba 2006 - Aidha,
aliwasili mkoani Mbeya(Tanzania) mwaka 2011 na kuitembelea taasisi ya
ARI UYOLE inayojihusisha na masuala ya uboreshaji wa kilimo na utafiti
katika nchi za Afrika
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN), Kofi Annan amefariki dunia akiwa na miaka 80 - Mwanadiplomasia huyo amefariki asubuhi ya leo nchini Uswisi baada ya kuugua kwa muda mfupi - Kutokana
na umahiri wake Kofi Annan alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa Desemba 1996. Na alianza kazi rasmi Januari 1, 1997 - Mwaka 2001 alichaguliwa kwa mara ya pili kuuongoza tena Umoja wa Mataifa. Oktoba 12, 2001 alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel - Annan
alianza kutumikia nafasi mbalimbali ndani ya Umoja wa Mataifa(UN) tangu
mwaka 1974 ingawa aliacha kazi na kurudi kuiongoza Kampuni ya Utalii
nchini mwake - Mwaka 1976 alirudi tena kwenye ulingo wa siasa za kimataifa na safari yake ndani ya Umoja wa Mataifa ikaanza rasmi - Kofi Atta Annan alizaliwa Aprili 8, 1938 nchini Ghana
Kampuni ya Johnson & Johnson imeamriwa na
Baraza la Mahakama kulipa dola bilioni 4.7 (takribani Tsh. Trilioni
10.7) kama fidia na faini kwa wanawake 22 waliodai kuwa bidhaa za
kampuni hiyo zimewasababishia saratani ya ovari
Katika kesi hiyo
iliyodumu wiki 6, wanawake hao na familia zao wamesema kuwa wamepata
saratani ya ovari baada ya kutumia poda ya Johnsons na baadhi ya bidhaa
zake
Mawakili wa familia hizo wamedai kuwa kampuni hiyo ilikuwa
inatambua kuwa bidhaa yao ya poda ya talc ilikuwa na madini mabaya ya
'asbestos' tangu mwaka 1970 lakini ilikosa kuwaonya watumiaji kuhusu
athari
Hata hivyo, Kampuni hiyo ilikana tuhuma hizo na
walisisitiza kwamba bidhaa hizo hazileti saratani. Nakuongeza kuwa
imesikitishwa sana na ina mpango wa kukata rufaa
Uamuzi huo unakuja wakati ambapo kampuni hiyo kubwa ya dawa ikipambana na kesi 9,000 zinazohusisha bidhaa yake maarufu ya poda
Aidha,
Mtaalumu wa mambo ya Afya, James Gallagher amedai kuwa kumekuwa na
wasiwasi kwa miaka kadhaa kwamba kutumia poda yenye madini ya talc au
talcum, hasa kwenye viungo vya uzazi, inaweza kuongeza hatari ya
saratani ya ovari lakini ushahidi haujakamilika
Kijana mmoja achapwa viboko 80 kwa kosa la kunywa pombe alilotenda akiwa na miaka 14
Aidha kijana huyo alitenda kosa hilo miaka 10 iliyopita na mpaka sasa haieleweki ni kwanini adhabu yake ilichelewa kutekelezwa
Shirika la Kimataifa la Amnesty limelaani adhabu hiyo iliyotekelezwa kwenye Mji ulio Mashariki mwa Jimbo la Kashmir
Ikumbukwe kuwa mwaka 2014, watu 6 walihukumiwa kwenda jela na viboko 91 baada ya kukutwa wakiuchezea wimbo wa Pharrel Williams.
Aidha,
mambo mengine yanayoweza kusababisha uchapwe viboko nchini Iran ni
pamoja na uzinzi, kubusu hadharani, wizi, vitendo vinavyohusiana na
mapenzi ya jinsia moja.
Waziri wa Mambo ya Nje, Boris Johnson ametangaza
kujiuzulu wakati nchi hiyo ikiwa kwenye mgogoro uliozuka katika
utekelezaji wa mpango wa kujiondoa kutoka katika uanachama wa Jumuiya ya
Ulaya 'BREXIT'
Boris anakuwa Waziri wa pili kujiuzulu ndani ya
saa chache baada ya Waziri aliyekuwa akishughulikia mpango wa BREXIT,
David Davis kujiuzulu
Mawaziri hawa wanajiuzulu wakati ambao
Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Theresa May anajiandaa kulihutubia Bunge
kuhusu mpango wake mpya juu ya BREXIT
Aidha, ofisi ya Waziri Mkuu imemshukuru bwana Boris na kuongeza kuwa mrithi wake atatangazwa haraka
Mtoto(Duduzane Zuma) wa Rais wa zamani, Jacob Zuma
ameshitakiwa kwa makosa ya rushwa katika Mahakama ya biashara mjini
Johannesburg.
Duduzane Zuma(34) anadaiwa kuwa sehemu ya
waliojaribu kumuhonga Naibu Waziri wa Fedha ili kumshawishi achukue
nafasi muhimu za juu kwenye Serikali. Mashitaka hayo pia yanahusishwa na
familia maarufu ya Gupta
Hata hivyo Duduzane pamoja na Familia ya Gupta wamekana kuhusika na mashitaka hayo
Mwaka
2015, Naibu Waziri wa Fedha, Mcebisi Jonas alidai kupewa ofa ya nafasi
ya Uwaziri wa Fedha na hongo ya 600 milioni rand(takirbani Tsh. Bilioni
100) wakati akiwa kwenye kikao na Duduzane, mfanyabishara Fana Hlongwane
na Ajay Gupta
Aidha, Duduzane ambaye anaishi Dubai alirejea
nchini humo ili kuhudhuria mazishi ya Kaka yake ndipo akakamatwa na hati
yake ya kusafiria kuchukuliwa
Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 24, 2019 na mshitakiwa yupo nje kwa dhamana
Serikali yatoa amri mpya ya kuwafukukuza kazi takribani watumishi wa umma 18,500 Amri hiyo itawagusa Askari wa Jeshi la Polisi, Wanajeshi na watumishi wa taasisi za elimu
Kwa
mujibu wa taarifa rasmi aliyotolewa katika gazeti la Serikali imeeleza
kuwa watumishi 18,632 idadi inayojumuisha maafisa wa polisi 8,998
Hatua
hizi zinachukuliwa ikiwa ni katika kusafisa Serikali baada ya taifa
hilo kunusurika katika mapinduzi yaliyopangwa na kukwama mnamo mwezi
Julai 2016
Wakati
wanandoa huko Wisconsin waliendesha kumkaribisha mtoto wao sio mama tu
alikuwa na usiku uliokumbwa na visanga bali baba pia alishiriki kwa njia
ambayo hakuwa ameitarajia.
Kujifungua kwake April Neubauer,
hakukuwa rahisi kwa sababu alikumbwa na tatizo linalofahamika kama
pre-eclampsia, na mpigo wa juu wa damu, hali iliyosababisha akimbizwe
chumba cha dharura cha upasuaji.
Wakati mtoto Rosalie alizaliwa
tarehe Juni 26, mama yake April alikumbwa na tatizo lingine ndipo
akapelekwa kwa matibabu zaidi kabla ya hata kumshika mtoto wake.
Kwa
sababu ya hilo mtoto Rosalie ambaye alikuwa na uzani wa kilo 3.6
akakabidhiwa baba yake Maxamilllian. "Muuguzi akaja na msichana wangu
mrembo , tukaenda chumba cha watoto, nikaketi na kuvua shati langu ili
nimkumbatie mtoto," aliiambia BBC.
Muuguzi akasema kuwa walihitaj
kumpa mtoto maziwa ya unga kwanza. "Kisha muuguzi akauliza kama
nitaweza kutoa titi langu nimnyonyeshe. Na mimi nikiwa mtu ambaye
anapenda kujaribu mambo, nikasema mbona nisifanye hivyo"
Muuguzi akaunganisha mrija ambao ulikuwa umeunganishwa na sirinji iliyokuwa na maziwa ya unga kwa kifua chake Maxamillian.
Mwanamke mmoja amelazwa katika hospitali ya Leratong baada ya kukutwa hai katika jokofu kwenye chumba cha kuhifadhia maiti
Mfanyakazi
katika chumba hicho aligundua bado mwanamke huyo anapumua wakati
alipofika kuutizama mwili na kutayarisha nyaraka kumhusu
Mwanamke
huyo alifikishwa katika chumba hicho baada ya madaktari kusema
amefariki kutokana na kutoonesha dalili zozote za uhai kufuatia ajali ya
barabarani aliyoipata
Familia ya mwanamke huyo imesema wamepata
mshtuko mkubwa na wana wasiwasi kuhusu mkasa huo hivyo wanahitaji
ufafanuzi ni vipi makosa hayo yanaweza kutokea
Taarifa ya furaha iliwafikia Wakenya kuwa Mwanamama tajiri duniani, Oprah Winfrey ataikanyaga ardhi yao kwa mara ya kwanza.
#Oprah
alitajwa kuwepo kwenye msafara wa ugeni wa Rais wa zamani wa Marekani
Barack Obama ambaye ametajwa kuwasili nchini Kenya Julai 16 mwaka huu
kwa shughuli mbili: Kuitembelea ikulu ya Kenya ambapo atatunukiwa tuzo
ya heshima pia baadae atakuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya Uzinduzi wa
NGO ya dada yake, Dr. Auma Obama itakayo fanyika kijijini kwao, K'Ogelo.
Sasa
taarifa rasmi kutoka kituo cha Televisheni cha CNN zimeripoti kuwa,
Oprah Winfrey hatokuwepo na taarifa zile za awali zilikuwa ni uzushi
mtupu "But it's not accurate that Oprah will go (Just to be clear on
that, since it's been a widely circulated rumor) " ilisomeka email ya
msemaji wa Obama.
Lakini kifuta machozi ni kuwa, ugeni huo
unatarajiwa kuchagizwa na uwepo wa Muimbaji mwenye asili ya Senegal,
AKON pamoja na mkongwe wa muziki kutoka nchini Zimbabwe, Oliver
Mutukudzi.
Kampuni moja Marekani yajitolea kugawa ticket za show ya Beyonce na JAY-Z kwa wote ambao watakubali kupima HIV
Kampuni
ya kujitolea inayotoa huduma za afya kupitia kituo cha Palmetto
Community Care imekuja na kampeni ya kuhimiza watu kwenda kujua afya
zao, imetangaza kuwa itakuwa inagawa ticket za show za #Beyonce na #JAY-Z kwa watu ambao watajitolea kwenda kupima Hii
kampuni ina gari la huduma ambalo linazunguka sehemu mbalimbali kama
vituo vya mabasi, club za usiku, kwenye matamasha na matukio mbalimbali
kuwafata watu ambao wataamua kupima kwenye mji wa South Carolina,
Marekani