Wizara ya mambo ya nje ya
Marekani imemwongeza kiongozi wa kundi la Hamas la Palestina Bw. Ismail
Haniyeh kwenye orodha yake ya magaidi wa kimataifa. Jana kundi la Hamas
limelaani uamuzi huo wa Marekani na kuutaja kuwa ni "hatua ya
kuchekesha". Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Hamas Bw. Hazem Qassem
amesema hili ni jaribio lililoshindwa la kushinikiza kukomesha mapambano
ya kisilaha ya wapalestina, na kwamba hatua hiyo haitavunja dhamira yao
ya kuendeleza mapambano hadi ukaliaji wa Israel kwenye ardhi ya
Palestina utakapokomeshwa.
0 comments:
Post a Comment