Tuesday 27 March 2018

Marekani yawafukuza wanadiplomasia 60 wa Urusi



Rais Trump ametoa amri ya kufukuzwa kwa wanadiplomasia 60 wa Kirusi, kufuatia Urusi kuhusishwa na shambulio la sumu kwa Jasusi wa zamani raia wa Urusi nchini Uingereza

Tayari nchi za kadhaa za Ulaya zikiwemo Ujerumani, Ufaransa na Ukraine zimetangaza kuwafukuza wanadiplomasia wa Kirusi katika nchi zao


Viongozi wa EU walikubaliana wiki iliyopita kuwa inawezekana sana Urusi ilihusika katika shambulio la sumu la Sergei Skripal(Jasusi) na binti yake kusini mwa Uingereza


Hata hivyo, Urusi imepinga kuhusika na shambulio hilo

0 comments:

Post a Comment