Serikali
ya Uturukiimetoa Jumatatu hii waranti wa kukamatwa kwa walimu 107 kwa
madai ya kuwa na uhusiano na kiongozi wa kidini alie uhamishoni,
Fethullah Gülen, ambaye Ankara inamshtumu kuchochea jaribio la mapinduzi
lililotibuliwa mwezi Julai 2016, shirika la habari la Uturuki, Dogan,
limearifu.
Walimu hamsini na
mmoja walikamatwa katika mji wa Ankara, Dogan limeaandika, likiongezea
kuwa operesheni inaendelea kuwaweka nguvuni wengine.Walimu hawa walikuwa wamesimamishwa kazi katika operesheni ya kamata kamata iliyofuata baada ya jaribio kushindwa, shirika hilo lilisema.
Watu zaidi ya watu 50,000 wamewekwa kizuizi kwa kusubiri kuhukumiwa kwa shutma ya kujaribu au kuungana moja kwa moja na jaribio hilo, na watumishi wa umma 150,000, walimu au wanajeshi wamefukuzwa au kusimamishwa kazi tangu mwezi Julai 2016.
Fethullah Gülen anachukuliwa na Uturuki kama adui wao nambari moja. Bw Gulen yuko uhamishoni nchini Marekani.
0 comments:
Post a Comment