Wednesday 13 December 2017

Mugabe aondoka Zimbabwe tangu ajiuzuru

Mugabe

Haki miliki ya picha
Aliyekuwa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameondoka nchini humo kwa mara ya kwanza tangu alipoondolewa madarakani na jeshi.
Bw Mugabe amesafiri kwenda Singapore kwa matibabu.
Kwa mujibu wa maafisa wa usalama wa serikali ambao wamezungumza na Reuters, Mugabe, 93, aliondoka nchini humu kwa ndege kutoka mjini Harare.
Aliandamana na mke wake Grace na wasaidizi kadha.
Anatarajiwa kutua mjini Malaysia ambapo binti Bona yupo akiwa mjamzito.
Mugabe, aliyekuwa ameongoza taifa hilo kwa miaka 37, alijiuzulu baada ya jeshi likishirikiana na baadhi ya maafisa wakuu wa chama tawala cha Zanu-PF kumgeuka ilipobainika kwamba alikuwa anamuandaa Grace, 52, awe mrithi wake.

0 comments:

Post a Comment