Kiongozi wa chama cha UKIP nchini
Uingereza Henry Bolton anasema kuwa amesitisha uhusiano na mpenzi wake
baada ya yeye kuripotiwa kutoa maoni ya ubaguzi wa rangi kumhusu Meghan
Markle.
Alisema kuwa mapenzi yao hayataendelea akiwa na wajibu kama kiongozi wa chama lakini hana nia ya kujiuzulu.Jo Marney alikuwa ametuma ujumbe wa simu kuwa watu weusi wana sura mbaya na mpenzi wake Prince Harry ataichafua familia ya kifalme.
0 comments:
Post a Comment