Friday 5 January 2018

Kitabu cha kashfa za Trump sasa kuingia mtaani

Mchapishaji wa kitabu chenye utata kuhusiana na rais Donald Trump amesema kuwa amevikabili vikwazo kutoka kwa wanasheria wa Trump wanaojaribu kusogeza mbele tarehe ya kuchapishwa kwa kitabu hicho na kusema sasa kinachapishwa leo hii siku ijumaa.


Kitabu hicho kijulikanacho kwa jina la Fire and Fury kilichoandikwa na Michael Wolff kutokana na upinzani mkali wa uchapishwaji wake kwa sasa kinatolewa siku nne kabla ya muda uliotarajiwa.
Mwandishi wa kitabu hicho amethibitisha kupitia ukurasa wake wa twita kwamba kitabu hicho kitakuwa mtaani leo. "kwa sasa mambo tayari,mtakisoma kesho.Asante sana Trump"ni nukuu ya mwandishi huyo wa kitabu.
Maoni ya mambo yanayomhusu rais Trump na familia yake yaliyozungumzwa ndani ya kitabu hicho,yametolewa na aliyekuwa msaidizi wa Trump Steve Bannon,zikiwemo tuhuma familia ya Trump kukutana na watu kutoka Urusi ili kuingilia masuala ya uchagauzi.

0 comments:

Post a Comment