Nchi sita za Afrika zimepewa
tuzo ya kuwa na maendeleo makubwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa
Malaria, wakati bara la Afrika linajitahidi kutimiza lengo la kukomesha
Malaria ifikapo mwaka 2030.
Madagascar, Senegal, Gambia na Zimbabwe zimepewa tuzo kutokana na kufanikiwa kupunguza asilimia zaidi 20 ya Malaria kati ya mwaka 2015 hadi mwaka 2016. Algeria na Comoro zimetuzwa kutokana na kukaribia kutimiza mkakati wa kiufundi wa kimataifa GTS uliowekwa na Shirika la Afya duniani WHO na kupunguza Malaria kwa zaidi ya asilimia 40.
Tuzo hizo zimetolewa na muungano wa kupambana na Malaria wa viongozi wa Afrika chini ya mfumo wa mkutano wa 30 wa kilele wa Umoja wa Afrika.
Madagascar, Senegal, Gambia na Zimbabwe zimepewa tuzo kutokana na kufanikiwa kupunguza asilimia zaidi 20 ya Malaria kati ya mwaka 2015 hadi mwaka 2016. Algeria na Comoro zimetuzwa kutokana na kukaribia kutimiza mkakati wa kiufundi wa kimataifa GTS uliowekwa na Shirika la Afya duniani WHO na kupunguza Malaria kwa zaidi ya asilimia 40.
Tuzo hizo zimetolewa na muungano wa kupambana na Malaria wa viongozi wa Afrika chini ya mfumo wa mkutano wa 30 wa kilele wa Umoja wa Afrika.
0 comments:
Post a Comment