Thursday 11 January 2018

Serikali ya Ethiopia yatoa katazo la raia wa kigeni kuasili watoto wa Ethiopia

Serikali ya Ethiopia imeanza rasmi kuweka katazo kwa raia wa kigeni kuasili watoto wa Ethiopia kwa madai kuwa watoto hao hunyanyaswa na kutelekezwa wakiwa ughaibuni.
Ethiopia ni miongoni mwa nchi ambazo ni vyazo vikuu vya watoto wanaoasiliwa na raia wa Marekani kwa kiwango cha kufiki asilimia 20 kwa kwa ujumla.
Watu maarufu kama Brad Pitt na Angelina Jolie ni miongoni mwa walioasili watoto kutoka Ethiopia.
Hata hivyo, mwaka 2013, wanandoa wawili kutoka marekani walishtakiwa kwa kumuua binti mmoja wa Ethiopia waliyekuwa wamemuasili. Kesi ambayo ilileta mjadala mkali nchini Ethiopia.
Mchakato mzima wa kuasili watoto nchini Ethiopia umekumbwa na maswali mengi asasi za kutetea haki za binadamu wakisema kuwa unawanufaisha wafanyabiashara wanaosafirisha binadamu.
Miaka miwili iliyopita , Denmark ilisitisha kuasili watoto kutoka Ethiopia.
Watunga sheria wa nchi hiyo wanasema kuwa yatima na watoto wote wasiojiweza wanatakiwa kutunzwa chini ya msaada utakao patikana nchini Ethiopia kwa ajili ya kuwalinda.
Ingawa baadhi ya wabunge wanasema nchi hiyo bado haina huduma bora inayoweza kuwapa uangalizi mzuri watoto hao wenye uhitaji.
Tangu mwaka 1999, watoto zaidi ya 15,000 wameasiliwa Marekani kutoka Ethiopia.
Wengine wengi wakiwa wanapelekwa katika nchi za ulaya kama Hispania, Ufaransa na Italia.

0 comments:

Post a Comment