Sunday 25 March 2018

Harusi ya Binti wa Dangote yakutanisha matajiri,watu mashuhuri



 Sherehe ya kifahari ya binti wa Bilionea namba moja Afrika, Aliko Dangote aitwaye Fatima Dangote, yazua gumzo nchini humo kutokana na kuhudhuriwa na watu mashuhuri kutoka sehemu mbalimbali duniani akiwemo Bilionea kutoka Marekani, Bill Gates.

Naye Rais Mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete alikuwa ni miongoni mwa wageni wa heshima waliohudhuria katika sherehe hiyo ya kihistoria.

Wengine walioudhuria ni pamoja na mke wa Rais wa sasa wa Nigeria, Hajiya Aisha Buhari; Makamu wa Rais, Osinbanjo; Spika wa Bunge, Magavana na Watu wengine mashuhuri wakiwemo wasanii na wafanyabiashara wakubwa.

Tafrija hiyo ya mapokezi baada ya ndoa (reception) kati ya Fatima na mumewe ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, Jamilu Abubakar, ilifanyika jana Ijumaa katika Jiji la Lagos.

0 comments:

Post a Comment