Mwingereza
Mo Farah alimshinda Mkenya Daniel Wanjiru na kushinda mzunguko wa
kwanza wa mbio za nusu marathoni za London, huku Callum Hawkins
akimaliza katika nafasi ya tatu.
Bingwa huyo mara nne wa Olimpiki alishiriki kwenye mbio hizo za nusu
marathoni kujiandaa kwa mbio za marathoni za London zitakazoandaliwa
mwezi Aprili. Farah mwenye umri wa miaka 34 ananuia kuwa mwanariadha wa
kwanza wa Uingereza kushinda mbio za wanaume tangu mwaka 1993.
0 comments:
Post a Comment