Pambano lililofanyika katika viwanja vya Cardiff nchini Wales, huku bondia Dillian Whyte wa Uingereza alifanikiwa kupata ushindi kwa njia ya pointi dhidi ya mpinzani wake Joseph Parker wa New Zealand.
Whyte alishinda kwa wingi wa pointi, kulingana na majaji akipata
113-112, 115-110, 114-111, na bondia huyo kwa sasa anatazamiwa kuanza
maandalizi ya kuwania mikanda ya uzito wa juu dhidi ya Deontay Wilder wa
Marekani au Anthony Joshua wa Uingereza.
Kwa upande wa mapambano ya Utangulizi, mwanadada Katie Taylor kutoka Ireland ya Kaskazini alimshinda Kimberley Connor wa Marekani kwa KO katika raundi ya tatu, na bondia huyo sasa amefanikiwa kutetea mataji yake ya ubingwa wa IBF na WBA.
Kwa upande wa mapambano ya Utangulizi, mwanadada Katie Taylor kutoka Ireland ya Kaskazini alimshinda Kimberley Connor wa Marekani kwa KO katika raundi ya tatu, na bondia huyo sasa amefanikiwa kutetea mataji yake ya ubingwa wa IBF na WBA.
0 comments:
Post a Comment