Polisi wametumia maji ya kuwasha na mabomu ya machozi ili kuwatawanya Waandamanaji huku ndege za kijeshi zikizunguka angani.
Hayo yametokea baada ya maelfu ya waandamanaji kudai kuwa uchaguzi uliofanyika umekuwa sio wa haki
-
Maandamano
hayo yamefanyika nje ya makao makuu ya Tume ya Uchaguzi nchini
humo(ZEC) ambayo inashutumiwa na wafuasi wa upinzani kuwa inaegemea
upande mmoja kwenye uchaguzi huo
-
Waandamanaji wengine
wameonekana kuwataka Rais Emmerson Mnangagwa na Makamu wake Constantino
Chiwenga(Mkuu wa Jeshi wa zamani), kuachia ngazi mara moja
-
Wafusi
wa vyama vilivyoshiriki katika uchaguzi huo wa kihistoria siku ya
Jumatatu wamekuwa wakionyesha hali ya kuchoka katika usubiriaji wa
matokeo ya Urais
0 comments:
Post a Comment