Sunday 26 November 2017

2 wafariki katika mlipuko mkubwa China


Maafisa nchini China wanasema watu wawili wamefariki na 30 wakajeruhiwa katika mlipuko kwenye kiwanda kimoja mjini Ningbo, kusini mwa Shanghai.
Mlipuko huo umesababisha vifo vya wawili na wengine wengi wakajeruhiwa.
Madirisha ya majengo yaliyo umbali wa hadi kilomita moja kutoka eneo la mlipuko yamepasuka.
Inakisiwa kuwa mitungi ya gesi imesababisha mlipuko huo, japo polisi wanaendelea na uchunguzi.
Picha zilizotolewa zinaonyesha wafanyikazi wa mjego wakiondoa watu kutoka kwenye eneo la mlipuko ambapo majengo yameharibiwa na magari yamebondwa.
Ambulensi zimeonekana zikiondoa watu kutoka kwenye eneo la mlipuko hadi kwenye hospitali zilizo karibu.
Mji wa Ningbo unajulikana kwa viwanda vya kutengeneza magari.

0 comments:

Post a Comment