Monday 4 December 2017

Jordan imekataa pendekezo la Marekani juu ya Jerusalem kuwa mjii mkuu Israel

Ayman Safadi alisema alimuambia waziri wa mashauri wa nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson kuwa hatua kama hiyo inaweza kuzua ghadhabu kubwa kwa nchi za kiarabu na ulimwengu wa kiisalmu.
Kuna uvumi kuwa Rais Donald Trump atatangaza hilo hivi karibuni na kutimiza ahadi yake aliyotoa wakati wa kampeni.
Jared Kushner, mkwe wa Trump alisema kuwa bado hakuna uamuzi uliofanywa.

Katika mtandao wa Twitter, Bw Safadi alisema: #Nilizungumza na waziri Rex Tillerson kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Hatua kama hiyo inaweza kusababisha ghadhabu kwenye nchi za kiarabu na kwa ulimwengi wa kiislamu na kuzua misukosuko na pia kuhujumu jitihada za amani."

I
Hakuna jibu lolote kutoka kwa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Marekani.
Naye rais wa Palestina Mahmoud Abbas anajaribu kupata uungwaji mkono wa kimataifa katika kumshawishi Trump asifanye tangazo kama hilo.
Ofisi yake ilisema kwa aliwapigia simu Jumapili viongozi wa dunia wakiwemo rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

"Alitaka kulezea harari za uamuzi wowote wa kuhamisha ubalozo wa Marekani kwenda Jerusalem au kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Isael," mshauri wa Bw. Abbas, Majdi al-Khalidi aliliambia shirika la AFP.Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Jardan ameonya Marekani kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

0 comments:

Post a Comment