Ni kweli Angela Merkel anashindwa na mambo kadhaa,
lakini bado anaongoza dhidi ya wanasiasa wengine nchini Ujerumani Angela
Merkel anaendelea kuwa na sifa ya kuwa kansela bora zaidi wala
hajatokea mpinzani
Miaka kumi na mbili iliyopita kansela Angela Merkel aliibuka kuwa
kansela wa kwanza mwanamke nchini Ujerumani. Na hadi sasa kama
kusingetokea matatizo katika kuunda serikali ya umoja baada ya
kumalizika uchaguzi bibi Merkel angelikuwa ni kansela aliyechaguliwa kwa
mara ya nne lakini baada ya kuvunjika kwa mazungumzo ya kuunda serikali
ya umoja na vyama vingine bibi Merkel anakosa wingi wa viti ndani ya
bunge la Ujerumani "Bundestag”.Hali hii naweza kuonekana kana kwamba mgogoro unanukia au nguvu ya Merkel inapungua. Lakini wala haionyeshi hali kuwa imefikia mahala hapo hasa wakati bibi Merkel pale alipotembea ndani ya bunge, na kupena mikono na wabunge. Na mara alipomuona na kumpungia mkono Paul Ziemiak, mwenyekiti wa tawi la vijana la chama chake cha CDU na baadae wawili hao wakaketi pamoja nyuma ambako kulikuwa hakuna watu na wakafanya mazungumzo ya faragha.
Mwenyekiti wa tawi la vijana la CDU Paul Ziemiak
Ziemiak
na wafuasi wake mara nyingi katika siku zilizopita walikuwa wakimlaumu
Kansela Angela Merkel lakini kwa sasa wanaonekana kuwa wamebadili
mawazo yao na kuunga mkono kauli zinazoashiria kuwa bibi Merkel ndiye
chaguo zuri katika kuiongoza nchi: anasema "Ujerumani inahitaji utulivu,
na kama kuna mtu anayesimama utulivu, basi mtu huyo ni Angela Merkel. "Lakini maneno hayo siyo waliyokuwa wakiyasema siku za hivi karibuni baada ya uchaguzi wa Septemba 24.Chama cha Christian Democtarac Union (CDU) pamoja na chama ndugu cha Christian Social Union (CSU) vyama hivyo vilipata asilimia 33 tu ya kura,hayo yakiwa ni matokeo yao mabaya kabisa tangu 1949.
Kutokana na kitisho hicho cha kupoteza umaarufu tawi la vijana wa CDU lilisema kuwa chama hicho kimepoteza uaminifu wake. Vijana wa tawi la CDU walisema ahadi kuu katika uchaguzi ya muendelezo na utulivu, haitoweza tena kutekelezwa. Lakini Kansela haoni sababu yoyote ya kujilaumu kwa kushindwa kwenye uchaguzi.
Andreas Rinke, mwandishi wa habari na shirika la habari la Reuters ambaye yuko mjini Berlin mesema Merkel anaona mambo tofauti kabisa na taswira iliyopo, yaani kwa mtazamo wake anaona kuwa matokeo ya uchaguzi yalikuwa si mazuri lakini sio mabaya. mwandishi huyo amekuwa akifuatilia hatua za Merkel kwa miaka mingi na mnamo mwaka 2016 alitoa kitabu kinacho muhusu kansela Merkel : "Das Merkel-Lexikon: Die Kanzlerin von A-Z" yaani ufafanuzi wa Merkel kuhusu Ukansela kutoka A mpaka Z.
Katika kitabu hicho cha Rinke, neno "kushindwa" lina sehemu yake kwenye ukurasa na mwisho wake kuna mstari unaosema: "Kwa Merkel, kushindwa si sawa na kushindwa kabisa na wa mwisho."
0 comments:
Post a Comment