Binti mmoja ambaye
ni mwanamitindo wa kibinafsi ambaye ametajwa kama "mwanaharakati wa
emoji" Rayouf Alhumedhi ameandikisha historia ya digitalI, kwa kuundwa
kwa mchoro uitwao emoji ili kuwakilisha wanawake wanaovalia vazi la
heshima kwa wanawake waislamu la hijab.
Rayouf anasema kuwa
alichoshwa kwa kushindwa kujitambua katika majukwaa ya kimataifa katika
picha na alama zake za vidole: ''Kujihisi kutengwa, sio uhalisia wa
kweli.....ni kama jambo ambalo ningependa liwepo au ninaloweza
lifanyike'.Hadi pale kampuni ya Apple, ilipotoa emoji hiyo, sikujua ninavyohisi,....
Mimi nina kwenda kuwa mwenye furaha kubwa. Naweza hata kufa kwa furaha niliyo nayo....!"
Akizungumza na chombo cha BBC ya The Cultural Frontline, kuhusu namna, kupitia kazi ya uchoraji wa grafiki na ubunifu wa kisasa, kupitia mtindo wa Aphee Messer, emoji hiyo ya hijabi ikazaliwa.
Msichana huyo raia wa Saudia anayeishi Ujerumani, amebuni emoji hiyo ya ijab kwa wanawake waislamu.
Rayouf Alhumedhi, ana umri wa miaka 15, na ametuma pendekezo hilo lake hadi kwa The Unicode Consortium, shirika moja la kibinafsi lisilohitaji faida yoyoye, ili emoji hiyo mpya ipigwe msasa, liundwe na kunakifishwa kabla ya kuanza kutumika.
Ikiwa itaidhinishwa, bila shaka itaanza kutumika mwaka huu wa 2017.
Kuna tofauti gani kati ya hijab, niqab and burka?
Mapendekezo hayo yanatukia wakati ambapo mataifa
kadhaa ya Bara Ulaya yanapoendelea kujadili swala la mavazi ya kiislamu
yanayofunika uso, kutumika kwa namna yoyote ile.
Mjadala huo unafanyika, chini ya Uhuru wa ibada, usawa wa kijinsia mingoni mwa wanawake, utamaduni wa kisasa na hofu ya kuongezeka kwa ugaidi duniani hasa wahanga wa kujitoa kufa.
Mjadala huo unafanyika, chini ya Uhuru wa ibada, usawa wa kijinsia mingoni mwa wanawake, utamaduni wa kisasa na hofu ya kuongezeka kwa ugaidi duniani hasa wahanga wa kujitoa kufa.
0 comments:
Post a Comment