Ofisi ya Taifa ya Takwimu kupitia
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Bw. Irenius Ruyobya imetangaza kushuka kwa mfumuko
wa bei nchini kutoka asilimia 5.3 hadi 5.1.
Mfumuko
wa bei wa taifa umeshuka kwa mwezi Oktoba, ikilinganishwa na ilivyokuwa
mwezi Septemba. Bw. Ruyobya ameeleza kuwa hiyo ina maana kwamba kasi ya
mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Oktoba
2017 imepungua ikilinganishwa na ilivyokuwa kipindi kama hicho mwaka
jana.
Ruyobya ameongeza kuwa kupungua huko kwa mfumko wa bei kumechangiwa na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Oktoba mwaka huu.
Aidha, Ruyobya amebainisha kuwa mfumko wa bei nchini unakaribiana na nchi nyingine za Afrika Mashariki ambapo nchini Kenya mfumko wa bei umepungua hadi asilimia 5.72 kutoka asilimia 7.06 huku nchini Uganda umepungua hadi asilimia 4.8 kutoka asilimia 5.3 kati ya mwezi Septemba na Oktoba.
Ruyobya ameongeza kuwa kupungua huko kwa mfumko wa bei kumechangiwa na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Oktoba mwaka huu.
Aidha, Ruyobya amebainisha kuwa mfumko wa bei nchini unakaribiana na nchi nyingine za Afrika Mashariki ambapo nchini Kenya mfumko wa bei umepungua hadi asilimia 5.72 kutoka asilimia 7.06 huku nchini Uganda umepungua hadi asilimia 4.8 kutoka asilimia 5.3 kati ya mwezi Septemba na Oktoba.
0 comments:
Post a Comment