Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania
Salum Mayanga ameweka wazi kuwa nafasi ya nahodha wa kikosi hicho Mbwana
Samatta itazibwa na wachezaji ambao amewaita ndani ya kikosi hicho.
Samatta
ambaye anakipiga kwenye ligi ya Ubeligji katika klabu ya KRC Genk
ameumia misuli ya paja hivyo kulazimika kukaa nje ya uwanja kwa
takribani wiki sita kwaajili ya matibabu.Hiyo inamaanisha Samatta
ataukosa mchezo wa Novemba 12 dhidi ya Benin.
Kocha Mayanga amekiri kuwa ni pengo kumkosa nahodha huyo lakini kama timu hawana budi kukubali na kutafuta namna ya kuziba nafasi yake kupitia wachezaji 24 ambao amewaita kwenye kikosi hicho.
“Ni kweli tumepata pengo kumkosa Samatta ambaye ni nahodha lakini hatuna namna lazima tukubaliane na hali halisi, lakini tunaowachezaji wanaoweza kuziba nafasi hiyo wakiwemo vijana tuliowaita kutoka timu za vijana”, amesema Mayanga.
Taifa Stars itasafiri kuelekea Benin ambako itacheza mchezo wa kalenda ya shirikisho la soka la kimataifa FIFA, Novemba 12.
Kocha Mayanga amekiri kuwa ni pengo kumkosa nahodha huyo lakini kama timu hawana budi kukubali na kutafuta namna ya kuziba nafasi yake kupitia wachezaji 24 ambao amewaita kwenye kikosi hicho.
“Ni kweli tumepata pengo kumkosa Samatta ambaye ni nahodha lakini hatuna namna lazima tukubaliane na hali halisi, lakini tunaowachezaji wanaoweza kuziba nafasi hiyo wakiwemo vijana tuliowaita kutoka timu za vijana”, amesema Mayanga.
Taifa Stars itasafiri kuelekea Benin ambako itacheza mchezo wa kalenda ya shirikisho la soka la kimataifa FIFA, Novemba 12.
0 comments:
Post a Comment