Kiongozi mkuu wa muungano wa NASA Raila Odinga leo amesma kuwa siku ya jumanne ambayo ndio itakuwa siku ya kumuapisha Rais Uhuru basi wao watakuwa wapo katika maombi ya kuwakumbuka wale ambao wamepoteza maisha yao siku ya uchaguzi na hata siku alivyowasili kutoka nchini Marekani. Maombi hayo ambayo yatafanyika katika viwanja vya Uhuru Park jijini Nairobi huku wakitaraji kuwa na wananchi kutoka pande tofauti nchini humo.Odinga aliongeza kwa kuwaomba polisi kutoingilia maombi yao kwani yatakuwa ni ya amani.
0 comments:
Post a Comment