Thursday 23 November 2017

ZIMBABWE KIONGOZI MPYA KUAPISHWA KESHO

Kiongozi mpya wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amesema nchi yake kwa inashuhudia mwanzo wa demokrasia mpya.



Mnangagwa, ambaye anatarajia kuapishwa kushika wadhfa wa Urais wa nchi hiyo siku ya Ijumaa, amesema kipaumbele chake ni kujenga upya uchumi wa nchi hiyo na kuunda ajira mpya kwa idadi ubwa ya watu wasio na ajira.

Katika hotuba yake hiyo, aliyokolezwa na maneno yaliyokuwa yakitumika wakati wa vita vya uhuru wa nchi hiyo, Bwana Mnangagwa alilishukuru jeshi la nchi hiyo, ambalo liliingilia kati baada ya yeye kufukuzwa na Rais Robert Mugabe na kuweza kufanikisha hali iliyopo sasa kwa amani.

0 comments:

Post a Comment