Rapa kutoka nchini Marekani Kanye West ametambulisha kiatu kipya kutoka kwenye kampuni yake ya mavazi ya Yeezy.
Kanye West ameonekana kwa mara ya kwanza akiwa
amevalia raba aina ya Yeezy 700 Nyeupe na Grey kwa mbali, Viatu hivi
bado havijaingia sokoni, anavaa yeye kwanza.
Mtindo wa kwanza wa toleo hili la Yeezy Wave
Runner 700 ulitoka August 2017 na viliuzwa vyote ndani ya dakika chache
baada ya kuingia madukani na kupanda beio kutoka dola 300 mpaka kufikia
dola 900 ambazo ni sawa na milioni 2 za kitanzania.


0 comments:
Post a Comment