Ripoti iliyotolewa na watafiti kutoka jopo la washauri la Chuo cha Tegemeo nchini Kenya imesema, nchi hiyo inatakiwa kuongeza uwekezaji kwenye maghala ya kisasa, mfumo mzuri wa usafiri na elimu kwa wakulima ili kupunguza hasara inayotokea baada ya mavuno.
Watafiti hao wamesema, Kenya ni moja ya nchi zenye kiwango cha
juu cha uharibifu baada ya mavuno ya mahindi, ambao unazuia juhudi za
nchi hiyo kuwapatia chakula watu wake. Wamesema hasara hiyo inachangia
pakubwa katika upungufu wa chakula na lazima ikabiliwe ipasavyo kama
mkakati wa kutimiza lengo la usalama wa chakula.
Utafiti huo umebaini kuwa uharibifu mkubwa baada ya mavuno ya mahindi nchini Kenya unatokana na ukosefu wa maghala ya kisasa na mabadiliko ya hali ya hewa.
Utafiti huo umebaini kuwa uharibifu mkubwa baada ya mavuno ya mahindi nchini Kenya unatokana na ukosefu wa maghala ya kisasa na mabadiliko ya hali ya hewa.

0 comments:
Post a Comment