Monday 1 January 2018

Ashley Young wa Manchester United aanza mwaka na kufungiwa


 

Mchezaji Manchester United Ashley Young afungiwa na kulazimika kutocheza mechi tatu mfululizo baada ya kufungiwa na chama cha soka FA.

FA imemfungia mchezaji huyo  kufuatia kitendo chake cha kumpiga kwa kiwiko cha mkono Dusan Tadic wa Southampton katika mechi baina ya timu hizo mbili iliyoisha kwa sare ya kutofungana jumamosi iliyopita.
Tukio hilo halikuonwa na moja kwa moja na mwamuzi, lakini kamera za uwanjani hapo zilimnasa na kwa mujibu wa kanuni za FA analazimika kufungiwa.
Kutokana na adhabu hiyo, Young atakosa mechi ya ligi kuu leo dhidi ya Everton, pia mechi dhidi ya Derby County ya kombe la FA pamoja na mechi nyingine ligi kuu dhidi ya Stoke City

0 comments:

Post a Comment