Wednesday 24 January 2018

Rafael Nadal ashindwa kuendelea kwenye robo fainali



Mchezaji namba moja kwa viwango vya ubora wa mchezo wa Tennis duniani Rafael Nadal wa Hispania, jana amelazimika kuishia hatua ya robo fainali katika michuano ya Australia baada ya kuumia akicheza jana dhidi ya Marin Cilic wa Croatia. Licha ya kuwa Nadal alifanikiwa kucheza chini ya uangalizi wa madaktari bado kasi yake ilikuwa kubwa, jambo lililopelekea mechi hiyo iende hadi seti tano huku Cilic akiitumia nafasi hiyo vizuri.
Kwa ushindi huo, Cilic sasa atakutana na Kyle Edmund wa Uingereza katika mechi ya nusu fainali ambaye alishinda katika mechi yake ya jana alipocheza dhidi ya Grigor Dimitrov wa Bulgaria.

0 comments:

Post a Comment