Saturday 20 January 2018

Wanawake Kenya walalamika kufanyiwa unyanyasaji


 Wanawake kenya  wadai kubakwa baada ya kujifungua katika Hospitali ya Kenyatta. Wamelalamika kuwa wamekuwa wakiviziwa wakati wakitoka kunyonyesha Watoto.

Waziri wa Afya, ameagiza uchunguzi wa dharura ufanyike na ripoti kamili iwasilishwe kwake kufikia Jumatatu

Hata hivyo Uongozi wa Hospitali hiyo umezikana tuhuma hizo na kusema kuwa hakuna mgonjwa aliyewahi kulalamikia unyanyasaji huo

Afisa Mkuu wa Hospitali hiyo kubwa ameongeza kuwa taasisi hiyo imefungwa mfumo wa Kamera za Usalama(CCTV) na hakuna kisa hata kimoja kilichoripotiwa

0 comments:

Post a Comment