Kampuni ya facebook
imetangaza kuwa imebadili kampuni inayoipa habari, ili kukabiliana na
kile ilichotaja kama habari za uzushi na za kupotosha.
Afisa mkuu
mtendaji wa kampuni hiyo ya facebook, Mark Zuckerberg, amesema mtandao
wake sasa utakuwa ukiwauliza matumiaji wake ni vyanzo vipi vya habari
wanaamini zaidi na hivyo kuwapa nafasi ya kwanza.Waandishi wa habari wanasema kuwa kampuni hiyo ya facebook ambayo ina zaidi ya watumiaji bilioni mbili, inataka kusitisha usambazaji wa habari bandia na propaganda, baada ya mahusiano yaliyojawa na malumbano na mashirika ambayo yana misimamo mikali ya kisiasa.
Mapema mwezi huu, Mark Zuckerberg, alitangaza mabadiliko ya vyanzo vya habari ya kampuni hiyo, iliyonuiwa kuhimiza ujumbe zinazotumwa na familia na marafiki badala ya mashirika ya kibiashara na bidhaa
0 comments:
Post a Comment