Chama tawala cha Afrika Kusini ANC
kimethibitisha kuwa kitamwondoa madarakani rais Jacob Zuma wa nchi
hiyo. Katibu mkuu wa chama cha ANC Bw. Ace Magashule amewaambia
waandishi wa habari kuwa, uamuzi huo umefikiwa jana katika mkutano wa
Kamati Kuu ya ANC uliofanyika Johannesburg. Amesema kwa wiki kadhaa
sasa, chama hicho kimefanya mawasiliano na rais Zuma kumtaka aondoke
madarakani. Rais Zuma anatakiwa kutoa jibu lake hii leo. Ameongeza kuwa,
kimsingi rais Zuma amekubali kujiuluzu, lakini amependekeza apewe muda
wa kati ya miezi mitatu hadi sita.
0 comments:
Post a Comment