Tuesday 6 February 2018

Cameroon kuwa Mwenyeji wa Afcon 2019


Baada ya kuwepo kwa sintofahamu ya Cameroon kuwa wenyeji wa fainali za AFCON mwaka 2019 michuano ambayo inayotarajiwa kuanza June saba hadi Julai saba, kutokana na kutokuwepo kwa kimiundombinu mizuri na maswala ya uchumi kuweza kuandaa michuano hiyo , CAF ililazimika kufanya uchunguzi wa maandali zi hayo.
Baada ya CAF kumaliza kufanya uchunguzi hatimaye wametoa ruhusu kwa Cameroon kuendelea kufanya maandalizi kwa ajili ya michuano hiyo baada ya timu ya maafisa wa CAF kuridhishwa na maandalizi yanayoendelea nchini humo.
Juniour Binyam ni mwenyekiti wa kamati ya masuala ya habari wa CAF amethibitisha hilo na kusema kwamba CAF kwa sasa hawana mashaka juu ya maandalizi ya michuano hiyo na wanaona hadi kufika wakati huo Cameroon watakuwa tayari.

0 comments:

Post a Comment