Sunday 4 February 2018

Guardiola agoma kumlaumu Sterling kwa mechi dhidi ya Burnley


Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola amekataa kumlaumu Raheem Sterling kwa mkosi wa kikosi chake kushindwa kuilaza Burnley baada ya mshambuliaji huyo wa Uingereza kukosa nafasi ya pekee.
Huku ikiwa 1-0 na dakika 20 chini ya ushindi wao wa 23 msimu huu, Sterling alishindwa kucheka na wavu akiwa maguu sita baada ya kupata pasi nzuri kutoka kwa Kyle Walker.
Kisa hicho kilimfanya kuzomwa huku mchezaji huyo akitolewa mara moja kabla ya Johann Berg Gudmundsson kuisawazishia Burnley ikiwa zimesalia dakika nane.
Mkufunzi wa Burnley Sean Dyche alihisi kushindwa huko kwa Sterling kulibadilisha hali ya mechi hiyo.
Uwanja mzima ulianza kutushangilia.
Lakini Guradiola amesisitiza kuwa hakumtoa nje Sterling kwa sababu ya kukosa nafasi hiyo ya wazi.

0 comments:

Post a Comment