Wakati Neymar anayeichezea
Paris Saint Germain akiwa majeruhi, mkataba wake na kampuni ya vifaa vya
michezo ya Nike umevuja, mkataba wa Neymar na Nike unaonesha kila kitu
atakachopewa katika soka kuanzia sasa. Mwanzo Nike walikuwa wakimlipa
kiasi cha €40m kwa mwaka na sasa Nike wako tayari kumpatia Neymar
$1million kama atachukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Ballon D'or)
mwakani kama Bonus. Kiasi hiki ambacho Neymar atapewa na Nike kama
akichukua Ballon D'Or kitakuwa kikiongezeka kwa 100% kila mwaka
atakayobeba tuzo hiyo na hii ina maana kwamba hadi 2022 anaweza pokea
hadi bonus $4million. Nike hawajaishia hapo kwani bado wana mpunga mrefu
wameutenga kwa ajili ya mchezaji huyo wa Kibrazil katika michuano ya
kombe la dunia inayotarajiwa kuanza hivi karibuni nchini Urusi. Endapo
Neymar atabeba kombe la dunia Nike watamkabidhi kiasi cha $50,000 na
kama nyota huyo atamaliza michuano hiyo mikubwa zaidi duniani akiwa kama
mfungaji bora wa michuano hiyo atachukua $200,000.
0 comments:
Post a Comment