Monday, 19 March 2018

Putin ndani ya nafasi za juu katika uchaguzi


Raia wa Urusi wanapiga kura Jumapili hii katika uchaguzi wa rais ambamo rais wa sasa Vladmir Putin anao uhakika wa kushinda muhula wa nne. Putin aliekuwa madarakani kwa karibu miongo miwili, alipiga kura mjini Moscow.
"Nina uhakika kuwa mpango nilioupendekeza kwa nchi ni sahihi," Putin alinukuliwa akisema na shirika la habari la Interfax.
Uchaguzi huo unafanyika mnamo wakati mgogoro unafukuta kati ya Urusi kwa upande mmoja, na Uingereza na washirika wake kwa upande mwingine kuhusiana na matumizi ya sumu iliyotengenezwa nchini Urusi dhidi ya jasusi wa zamani na Uingereza na binti yake katika mji wa Uingereza wa Salisbury. Urusi imekanusha ushiriki wowote katika tukio hilo.
Uchaguzi huo pia unafanyika katika siku ya kumbukumbu ya mwaka wa nne tangu Urusi ilipoitwa rasi ya Crimea kutoka Ukraine, hatua ambayo ilichukuliwa na Urusi kama kichocheo kwa umaarufu wa Putin ambao tayari ulikuwa imara.
Ameendelea kuwa na umaarufu wa asilimia 70 katika miaka ya karibuni, kwa mujibu wa tafiti za maoni ya raia zilizofanyika nchini kote na mashirika mawili makubwa zaidi ya utafiti nchini humo, moja la kiserikali na lingine la binafsi.
Muda wa utawala wa Putin hata hivyo, umezusha uvumi kwamba wapigakura wengi huenda wakajizuwia kushiriki uchaguzi huu ambao matokeo yake yanaonekana kutabirika kwa kiasi kikubwa. Chini ya katiba kama ilivyo sasa, muhula wa nne ndiyo wa mwisho kwake.
Russland Wahlen (picture-alliance Donat Sorokin/TASS/dpa) Orodha ya wagombea urais kama ilivyoonekana wakati wa zoaezi la kupiga kura katika kituo cha kupigia kura. Kibao cha nyuma kinasomeka "Kwa ajili ya Urusi."
Uchaguzi huo ulipangwa kumalizika wakati vituo vya kupigia kura vitakapofungwa katika mkoa wa Kalinigrad ulioko mbali magharibi mwa Urusi majira ya mbili za usiku. Urusi ndiyo nchi kubwa zaidi duniani na inazo zoni 11 za wakati. Karibu wapigakura milioni 109 wana vigezo vya kupiga kura.
Mmoja wa wakosoaji wakubwa zaidi wa Putin, kiongozi wa maandamano Alexei Navalny, alizuwiwa kugombea katika uchaguzi huo kutokana na kutiwa hatiani kwa makosa ya kifedha, ambayo anayapinga kwa madai kuwa yalipangwa tu. Navalny aliwatolea mwito Warusi kususia uchaguzi huo na kueleza matumani kuwa utadhoofishwa na uitikiaji mdogo.
Wapinzani wakuu watatu wa Putin, kwa mujibu wa kura za maoni, walikuwa Pavel Grudini wa chama cha Kikomunisti, Mzalendo Vladmir Zhironovsky, na mwanahabri aliegeuka msoshalisti Ksenia Sobchak. Lakini wako nyuma kabisaa ya Putin wakiwa na umaarufu wa tarakimu moja tu katika utafiti wa maoni ya wapigakura.
Jaribio la udukuzi wa tovuti ya uchaguzi
Tume ya uchaguzi ya Urusi imesema tovuti yake ililengwa katika jaribio lililofeli la udukuzi wakati wa zoezi la upigaji kura la Jumapili. Mwenyekiti wa tume hiyo Ella Pamfilova aliwaambia waandishi habari kwamba jaribio hilo lilifuatliwa na kuhusishwa na kompyuta katika mataifa 15, bila kuyataja mataifa hayo. Mashambulizi kama hayo ni ya kawaida.
Alisema juhudi za kuvuruga tovuti hiyo zilitokea wakati wapigakura katika eneo la mbali la mashariki mwa Urusi wameanza kupiga kura, lakini zilizuwiwa na maafisa wa Urusi.
Wakati Marekani ikichunguza madai ya udukuzi wa Urusi na uingiliaji mwingine katika ushindi wa rais Donald Trump katika uchaguzi wa 2016, maafisa wa Urusi wamedai pia kwamba mataifa ya kigeni yanajaribu kuingilia uchaguzi wa Jumapili.

0 comments:

Post a Comment