Christiano
Ronaldo ameweka rekodi ya kufunga hat-trick ya 50 katika maisha yake
ndani ya Real Madrid baada ya kuichapa Girona magoli 6-3 katika mechi ya
ligi kuu ya Uhispania La Liga.
Ronaldo alifunga bao la kwanza kwa kumalizia pasi ya Toni Kroos,
Girona wakasawazisha na kufanya matokeo kuwa 1-1, Real Madrid ilifanya
mashambulizi na kuongeza magoli mawili moja likifungwa na Ronaldo tena,
Katika muda wa majeruhi, Christian Ronaldo aliongeza goli na kupiga
hat-trick. Madrid sasa wako pointi 15 nyuma ya vinara wa ligi hiyo
Barcelona.
0 comments:
Post a Comment