Rais wa shirikisho la soka
Tanzania (TFF) Wallace Karia amesema haya yanayotokea kwa sasa ndani ya
shirikisho hilo ni miongoni mwa matokeo ya utekelezaji wa taarifa za
timu ya uchunguzi kutoka shirikisho la soka duniani (FIFA).
Karia ameyasema hayo katika mkutano na waandishi wa habari jana
jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo mzima wa TFF, na kueleza kuwa
Makamu wake wa Rais Michael Wambura amefungiwa maisha kujihusisha na
masuala ya soka na kamati ya maadili ya shirikisho hilo kutokana na
makosa matatu ambayo ni kupokea fedha za TFF malipo yasiyo halali,
kughushi barua na kushusha hadhi ya TFF.
0 comments:
Post a Comment