Mtandao wa Twitter waungana na Google pamoja na washindani wake Facebook kupiga marufuku matangazo wa sarafu ya mtandaoni ikiwemo ya Bitcoin
Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kuibuka kwa wimbi kubwa la taasisi zinazotangaza sarafu zako hivyo ni ngumu kutambua taasisi ipi ni halisi na ipi inaendeshwa kitapeli
Twitter wamekiri kuwa matangazo ni moja ya vyanzo vikubwa vya mapato katika mtandao wao lakini wameamua kuchua hatua hiyo ili kuepusha madhara kwa watumiaji wake
Kufuatia marufuku hiyo sarafu maarufu ya Bitcoin imeshuka kwa asilimia 5 sawa Dola za Kimarekani 8,000(Tsh. Mil18)
Huku sarafu ya Ethereum ikishuka kwa 10.73% sawa na $456 na sarafu ya 6.63% sawa na $0.57
0 comments:
Post a Comment