Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN), Kofi Annan amefariki dunia akiwa na miaka 80
-
Mwanadiplomasia huyo amefariki asubuhi ya leo nchini Uswisi baada ya kuugua kwa muda mfupi
-
Kutokana
na umahiri wake Kofi Annan alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa Desemba 1996. Na alianza kazi rasmi Januari 1, 1997
-
Mwaka 2001 alichaguliwa kwa mara ya pili kuuongoza tena Umoja wa Mataifa. Oktoba 12, 2001 alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel
-
Annan
alianza kutumikia nafasi mbalimbali ndani ya Umoja wa Mataifa(UN) tangu
mwaka 1974 ingawa aliacha kazi na kurudi kuiongoza Kampuni ya Utalii
nchini mwake
-
Mwaka 1976 alirudi tena kwenye ulingo wa siasa za kimataifa na safari yake ndani ya Umoja wa Mataifa ikaanza rasmi
-
Kofi Atta Annan alizaliwa Aprili 8, 1938 nchini Ghana
0 comments:
Post a Comment