Ni
wimbo unaozungumzia jamaa aliyetelekezewa watoto na Mkewe Kisa na Mkasa
ni Ukata.. Hali Duni ya Maisha na Umasikini, Mwanamke huyo Akimbilia
kwa mabwana wenye pesa na Kuanza kuponda Raha... Huku Nyuma watoto
kawaacha wanalelewa na baba kiugumu huku kila siku watoto wanamuuliza
baba, Mama yu wapi?? Baba kishingo upande ana kaza moyo na Kuwaambia
ATARUDI.... Miaka 20 Baadae Jamaa anapata pesa na Kuwa tajiri na
hatimaye anaanzisha Maisha mapya... Ghafla Yule mwanamke alimkimbia
anarudi akiwa kapigika sana akitaka warudiane na baba watoto lakini
inakuwa ni too late... Watoto hawamtumbui mama na hawamtaki kabisa kwani
washakuwa watu wazima na Baba tayari Alishawasogeza kimaisha
0 comments:
Post a Comment