Thursday 13 September 2018

Hivi ndio vyuo vinavyopendwa sana na waajiri


University College London ni cha 18. Kwa kuangazia sifa za vyuo vikuu miongoni mwa waajiri, Cambridge na Oxford ndivyo vinavyoongoza, lakini kwa jumla vyuo vikuu vya Uingereza vilishuka katika ushirikiano na waajiri na viwango vya kuajiriwa kwa wanafunzi wao.
Kuimarika kwa China kunadhihirishwa na kuorodheshwa kwa Tsinghua University nafasi ya tisa na University of Peking nafasi ya 20.

Kati ya vyuo vikuu 500 vilivyoorodheshwa, 102 vinatoka bara Asia, 144 kutoka Ulaya Magharibi. Marekani ina vyuo vikuu 83, ambapo 13 kati ya vyuo hivyo vimo katika orodha ya 30 bora. Afrika kuna vyuo vikuu 10.
Chuo hicho kikuu cha Nairobi ndicho pekee kutoka Afrika Mashariki ingawa kimeshuka kutoka nambari tano Afrika mwaka 2018, mwaka ambao kulikuwa na vyuo vikuu 11 vya Afrika katika vyuo vikuu 500 bora duniani kwenye orodha hiyo.
Vyuo Vikuu vinavyopendwa na waajiri Afrika 2019
  1. University of Cape Town, Afrika Kusini
  2. The American University in Cairo, Misri
  3. University of Witwatersrand, Afrika Kusini
  4. Cairo University, Misri
  5. Ain Shams University, Misri
  6. Stellenbosch University, Afrika Kusini
  7. University of Johannesburg, Afrika Kusini
  8. University of Kwazulu-Natal, Afrika Kusini
  9. University of Nairobi, Kenya
  10. University of Pretoria, Afrika Kusini
Chuo kikuu cha Alexandria cha Misri ndicho kilichotupwa nje katika orodha ya mwaka huu baada ya kuwa nambari nane Afrika mwaka uliopita.
Chuo kikuu cha Cape Town ambacho kinaongoza Afrika katika orodha ya jumla kinashikilia nafasi ya 101-110, na hakuna chuo kingine cha Afrika hadi baada ya vyuo mia ambapo ndipo unapata chuo kikuu cha Kimarekani cha Cairo na Chuo Kikuu cha Witwatersrand cha Afrika Kusini katika nafasi ya 201-250.
Chuo Kikuu cha Nairobi kinashikilia nafasi ya 301-500. Mwaka jana, kilikuwa katika nafasi ya 251-300 kwa jumla.
Mwaka 2017, Afrika ilikuwa na vyuo vikuu vinne pekee, wakati huo orodha hiyo kwa jumla ikishirikisha vyuo vikuu 300 duniani. Mwaka 2017 walishirikisha vyuo 494 na mwaka huu vyuo 497.


0 comments:

Post a Comment