Friday 27 October 2017

Joti kufunga Ndoa karibuni

Mchekeshaji mkongwe wa Tanzania , Joti hatimaye ameamua kuachana na  ukapera na sasa rasmi  kudai anaoa na kuamua kufanya kweli kwa kudhihirisha yupo serious kidogo kwa jambo la mahusiano kwa kutarajia kuvuta jiko hivi karibuni.


Joti ambaye anafahamika kwa kufanya matangazo mengi ikiwemo ya kufunga ndoa , aliambatana na  watu wake wa karibu  katika sendoff  yake  iliyofanyika siku ya jana( Alhamisi) akiwa na mchekeshaji Seki.





Mchekeshaji huyo mwenye dili kibao town anatarajia kufunga ndoa rasmi  hivi karibuni na atakuwa ameingia kwenye orodha ya mastaa wa Bongo waliopo  katika ndoa kama Babuu wa Kitaa, Mx Carter, Kenedy The Remedy, Professa Jay, ZamaradI Mketema na Frola Mbasha.

0 comments:

Post a Comment