Serikali ya shirikisho la Ujerumani imejitolea kuunga mkono Umoja wa Afrika katika juhudi zake za kutoa mafunzo na ajira kwa vijana, na kwamba wametenga Euro milioni 28 kuimarisha maarifa barani Afrika
Afrika ndilo bara lenye idadi ya watu wenye umri mdogo zaidi duniani. Watu hao wanaweza kuleta mabadiliko ya kuboresha mustakabali wa Afrika ikiwa watapewa nafasi muhimu. Hayo yamesemwa na mwakilishi maalum wa kansela wa Ujerumani barani Afrika Guenter Nooke, katika mkesha wa mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya na Afrimka mjini Abdijan.
Kwenye mkutano wake na naibu mwenyekiti wa Muungano wa Afrika Kwesi Quartey, na mwenyekiti wa Biashara Afrika Albert Yuma, pembezoni mwa mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya na Afrika unaoanza kesho mjini Abidjan Cote d`Ivoire , mwakilishi huyo maalum wa Kansela wa Ujerumani Guenter Nooke.
Amesema serikali ya shirikisho la Ujerumani imejitolea kuunga mkono Umoja wa Afrika katika juhudi zake za kutoa mafunzo na ajira kwa vijana, na kwamba wametenga Euro milioni 28 kuimarisha maarifa barani Afrika na Euro milioni 3 kwa utekelezwaji wa sera ya uhamiaji ambayo pia inahusiana na ajira na uhamiaji.
0 comments:
Post a Comment