Waziri mkuu wa Lebanon Saad al-Hariri ametangaza kujiuzulu katika hatua ya kushangaza akisema kuwa anahofia maisha yake.
Amesema kuwa hali ya sasa nchini Lebanon ni sawa na ilivyokuwa wakati babake Rafiq alipouawa 2005 na kwamba alikuwa anahisi kuna njama ya kumuangamiza.
Waandishi wanasema kuwa ni muhimu kwamba bwana Hariri hakuwa akizungumza kutoka Beirut bali kutoka Saudia ambayo ni mkosoaji mkubwa wa Iran.
0 comments:
Post a Comment