Thursday 7 December 2017

FIFA yamteua Mtanzania Jonesia Rukyaa kuchezesha Kombe la Dunia nchini Ureno

 

Refa maarufu mwanamama Jonesia Rukyaa Kabakama ameteuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), kuchezesha fainali zijazo za Kombe la Dunia kwa wanawake (Algarve Cup) zitakazofanyika nchini Ureno, mwezi Februari, mwakani.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka TFF, Jonesia, ambaye ni mwanamke, ameteuliwa kupuliza filimbi katika fainali hizo ambazo hukutanisha timu mahiri zilizofanya vema katika michuano ya kila Bara.
Lakini kabla ya kwenda Ureno, Jonesia anatarajiwa kushiriki semina maalumu iliyoandaliwa na FIFA. Semina hiyo itafanyika Doha, Qatar kuanzia Februari 12- 16, mwakani.
Waamuzi wengine walioteliwa kutoka Afrika Lidya Abebe wa Ethiopia, Glady Lengwe wa Zambia na Salima Mukansanga wa Rwanda.

0 comments:

Post a Comment