Chama
cha Demokrasia na Maendeleo kimekanusha habari inayoenea kuhusu Mbunge
wa Kibamba, John Mnyika kujivua uanachama kuwa hazina ukweli wowote na
zinapaswa kupuuzwa.
Chadema
wametua kanusho hilo kupitia mtandao wa Twittter kwenye ukurasa wa
chama hicho na kusema kwamba wanaosambaza habari za Mnyika kujivua ni
wale walioishiwa hoja na majibu juu ya maisha ya watanzania.
"Kuna
taarifa zinasambazwa mitandaoni ya kuwa Mhe. John Mnyika, Mbunge wa
Kibamba amejivua uanachama wa CHADEMA. Taarifa hizo ni za uongo na
hazina ukweli wowote, ni za kupuuzwa, wanaozisambaza ni wale walioishiwa
hoja na majibu juu ya hali ya maisha ya Watanzania".
0 comments:
Post a Comment