Thursday 7 December 2017

NATO,Umoja wa Ulaya kuimarisha vita dhidi ya ugaidi, usalama


NATO na Umoja wa Ulaya zimeamua kuimarisha ushirikiano wao katika kupambana na ugaidi na kukuza majukumu ya wanawake. Hayo yameafikiwa katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa taasisi hizo mjini Brussels. Wakati huohuo waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson anayehudhuria mkutano huo amesema hakuna kurejesha hali ya kawaida kimahusiano na Urusi.
Ushirikiano kati ya nchi 28 wanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO ulikuwa miongoni mwa ajenda za kujadiliwa katika mkutano huo wa siku mbili, kando na mzozo kuhusu Korea Kaskazini na Urusi.
Katibu Mkuu wa NATO, Jenerali Jens Stoltenberg, amesema wanainua ushirikiano kati ya Umoja wa Ulaya na NATO katika ngazi zaidi.
NATO na Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuhusu hatua 32 ambazo zitaimarisha ushirikiano zikiwemo za kukabili ugaidi, kuhakikisha vifaa vya kijeshi na wanajeshi wanafikishwa kwa haraka ndani ya Ulaya na pia kuimarisha majukumu ya wanawake katika masuala ya amani na usalama.
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Federica Moghereni, amesisitiza kuwa uamuzi wa hivi karibuni wa kuimarisha ulinzi na usalama katika viwango vya Umoja wa Ulaya haukukusudia kubadilisha muungano wa EU kuwa muungano wa kijeshi, lakini ulimaanisha haja ya kuimarisha uwezo wa Umoja wa Ulaya kwa manufaa ya NATO pia.

0 comments:

Post a Comment