Nigeria wamepangwa
kwenye kundi moja na Argentina kwa mara nyingine, Misri nao wakapangwa
na Urusi na Uruguay baada ya droo ya Kombe la Dunia 2018 kufanywa nchini
Urusi.
Panama, ambao wanacheza Kombe la Dunia mara ya kwanza wamepangwa na Ubelgiji na England na Tunisia.Iceland, walioshangaza wengi kwa kufuzu, wamepangwa kucheza na Nigeria, Croatia na Argentina katika Kundi D.
Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Urusi na Saudi Arabia.
Droo kamili ya Kombe la Dunia:
- Kundi A: Urusi, Saudi Arabia, Misri, Uruguay
- Kundi B: Ureno, Uhispania, Morocco, Iran
- Kundi C: Ufaransa, Australia, Peru, Denmark
- Kundi D: Argentina, Croatia, Iceland, Nigeria
- Kundi E: Brazil, Uswizi, Costa Rica, Serbia
- Kundi F: Ujerumani , Mexico, Sweden, Korea Kusini
- Kundi G: Ubelgiji , Panama, Tunisia, England
- Kundi H: Poland, Senegal, Colombia, Japan.
0 comments:
Post a Comment