Friday 1 December 2017

Nigeria, Argentina watakutana tena Kombe la Dunia


Nigeria wamepangwa kwenye kundi moja na Argentina kwa mara nyingine, Misri nao wakapangwa na Urusi na Uruguay baada ya droo ya Kombe la Dunia 2018 kufanywa nchini Urusi.
Panama, ambao wanacheza Kombe la Dunia mara ya kwanza wamepangwa na Ubelgiji na England na Tunisia.
Iceland, walioshangaza wengi kwa kufuzu, wamepangwa kucheza na Nigeria, Croatia na Argentina katika Kundi D.
Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Urusi na Saudi Arabia.

Droo kamili ya Kombe la Dunia:

  • Kundi A: Urusi, Saudi Arabia, Misri, Uruguay
  • Kundi B: Ureno, Uhispania, Morocco, Iran
  • Kundi C: Ufaransa, Australia, Peru, Denmark
  • Kundi D: Argentina, Croatia, Iceland, Nigeria
  • Kundi E: Brazil, Uswizi, Costa Rica, Serbia
  • Kundi F: Ujerumani , Mexico, Sweden, Korea Kusini
  • Kundi G: Ubelgiji , Panama, Tunisia, England
  • Kundi H: Poland, Senegal, Colombia, Japan.

0 comments:

Post a Comment