Friday 19 January 2018

Australia-Johanna Konta wa Uingereza afungwa raundi pili



Mchezaji namba moja kwa viwango vya ubora wa tennis kwa upande wa wanawake nchini Uingereza Johanna Konta, jana amejikuta akiondolewa kwenye mashindano ya Australia baada ya kufungwa na mchezaji namba 123, Bernarda Pera wa Marekani. Konta ambaye ni namba tisa kwa ubora duniani alifungwa kwa seti 6-4 na 7-5 na hicho kikiwa ni kipigo cha 8 katika mechi 11 alizocheza tangu mwezi Julai mwaka jana.
Na kutokana na ushindi wa jana, Bernarda atakutana na Barbora Strycova wa Czech katika mechi ya raundi ya tatu.

0 comments:

Post a Comment