Tuesday 23 January 2018

Chama cha ANC Afrika Kusini chakanusha juu ya kumwondoa madarakani rais Zuma


Chama tawala cha Afrika Kusini ANC kimesema kimejadili suala la kumwondoa madarakani rais Jacob Zuma wa nchi hiyo, lakini hakuna ratiba iliyopangwa kufanya hivyo.
Katibu mkuu wa ANC Bw Ace Magashule amesema kamati tendaji ya taifa ya chama hicho haijafanya uamuzi wa kumwita na kumhoji rais Zuma, ambaye anashinikizwa kujiuzulu. Kamati hiyo imekubali kuhakikisha uratibu kati ya chama chake na serikali kuhusu jambo hilo.

0 comments:

Post a Comment