Waziri wa mambo ya nje wa
Ethiopia Bw. Workneh Gebeyehu amesema mapambano dhidi ya ufisadi
yatakuwa ni ajenda kuu ya mkutano wa 30 wa Umoja wa Afrika unaofanyika
mjini Addis Ababa.
Mkutano wa 30 wa Umoja wa Afrika ulioanza jumatatu na kuendelea hadi jumatatu wiki ijayo katika makao makuu ya Afrika mjini Addis Ababa, kauli mibu yake ikiwa ni "kushinda mapambano dhidi ya ufisadi, njia endelevu ya mabadiliko ya Afrika".
Akizungumza na waandishi wa habari, Bw Gebeyehu amesema kiwango cha ufisadi na mapambano dhidi yake kwa sasa vimekuwa kigezo muhimu cha kupima uwezo wa kitaasisi na utawala bora wa nchi moja. Pia amsema kutokana na kuwa asilimia 70 ya waafrika zaidi ya bilioni moja ni vijana, mapambano dhidi ya ufisadi ni mustakbali wa nchi za Afrika.
Mkutano wa 30 wa Umoja wa Afrika ulioanza jumatatu na kuendelea hadi jumatatu wiki ijayo katika makao makuu ya Afrika mjini Addis Ababa, kauli mibu yake ikiwa ni "kushinda mapambano dhidi ya ufisadi, njia endelevu ya mabadiliko ya Afrika".
Akizungumza na waandishi wa habari, Bw Gebeyehu amesema kiwango cha ufisadi na mapambano dhidi yake kwa sasa vimekuwa kigezo muhimu cha kupima uwezo wa kitaasisi na utawala bora wa nchi moja. Pia amsema kutokana na kuwa asilimia 70 ya waafrika zaidi ya bilioni moja ni vijana, mapambano dhidi ya ufisadi ni mustakbali wa nchi za Afrika.
0 comments:
Post a Comment