Saturday 20 January 2018

Merkel kukutana na Macron Paris juu ya sarafu ya Euro


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kukutana kujadili masuala ya kodi na bajeti ya nchi zinazotumia sarafu ya Euro
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel watakutana leo Ijumaa mjini Paris, Ufaransa kuangalia mipango ya kukubaliana kuhusu mageuzi katika eneo linalotumia sarafu ya Euro. Viongozi hao pia wanatarajiwa kujadili juu ya masuala ya kodi na bajeti ya ukanda huo wa Euro.
Viongozi hao wanatafuta kuwa na msimamo mmoja katika malengo ya mageuzi. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron wanatarajiwa kutumia muda wa zaidi ya saa  tano pamoja mjini Paris kuonyesha uwepo wa umoja baina ya Ujerumani na Ufaransa huku wakijaribu kukubaliana juu ya mageuzi katika ukanda wa Euro.
Kwenye mkutano wa kilele uliofanyika mjini Brussels mwezi uliopita, viongozi hao wawili walisema wanatumai kuleta mapendekezo  ya pamoja juu ya mageuzi katika nchi zinazotumia sarafu ya Euro hadi kufikia mwezi Machi. Macron anaweka mkazo juu  ya bajeti ya  kujitegemea pamoja na kuchaguliwa waziri wa fedha wa ukanda  huo.
Majadiliano na Ufaransa yachelewa
Juhudi za Kansela Merkel za kuunda serikali nchjni Ujerumani zimerudisha nyuma majadiliano na Ufaransa. Hata hivyo matumaini ya kuweza kuunda serikali ya mseto na chama cha Social Demokratic SPD yameutia msukumo mpya mjadala juu ya mageuzi katika nchi za ukanda wa sarafu ya Euro.
Ujerumani na Ufaransa ambazo kwa pamoja zinachangia asilimia 50 ya zao la ukanda hu

0 comments:

Post a Comment